Elihu Anazungumza na Ayubu
33 1"Lakini sasa, Ayubu, sikia maneno yangu; tega sikio kwa kila nisemalo. 2Tazama, nimeufumbua mdomo wangu; ulimi wangu waunda maneno kaakaani mwangu. 3Maneno yangu yatoka katika moyo mnyofu, na midomo yangu hunena kwa unyofu yale iyajuayo. 4Roho wa Mungu ndiye aliyeniumba, na pumzi ya Mwenyezi hunipa uhai. 5Nijibu, kama ukiweza; panga shauri lako mbele yangu, ukasimame imara. 6Tazama, mimi ni kama wewe mbele za Mungu; nami pia niliumbwa kwa udongo. 7Woga wangu usikutishe, wala shinikizo langu lisikuelemee.
8"Hakika umesema nikiwa nasikia—niliisikia sauti hasa ya maneno yako. 9'Mimi ni safi, bila uasi; nimetakasika, wala hakuna hatia ndani yangu. 10Lakini yeye anitafutia makosa; ananihesabu kuwa adui yake. 11Ayafunga miguu yangu katika mkatale; azichunga njia zangu zote.'
12"Lakini katika jambo hili huna haki, nakujibu, kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mwanadamu ye yote. 13Mbona unashindana naye, kwamba hajibu neno lo lote la mwanadamu? 14Kwa maana Mungu hunena kwa njia moja, kisha kwa njia nyingine, ingawa hakuna aitambuaye. 15Katika ndoto, katika maono ya usiku, usingizi mzito uwaangukiapo watu walalapo vitandani mwao, 16ndipo huyafunua masikio yao na kuyakaza maonyo yake juu yao, 17ili kumgeuza mtu na ubaya wake na kumzuia mwanadamu na kiburi, 18huizuia nafsi yake na shimo, na uhai wake usiangamie kwa upanga.
19"Mtu pia huonywa kwa maumivu kitandani pake, na uchungu wa daima katika mifupa yake, 20hata uhai wake huuchukia mkate, na nafsi yake huchukia chakula kizuri kabisa. 21Nyama yake hukonda, na mifupa yake, iliyokuwa imefichika, hutokeza. 22Nafsi yake hulisogelea shimo, na uhai wake huwakaribia wale waletao mauti.
23"Ikiwa yupo mjumbe kwa ajili yake, mpatanishi—mmoja katika elfu—wa kumtangazia mtu lililo sawa kwake, 24naye anamhurumia na kusema, 'Mwokoe asishuke shimoni; nimepata fidia,' a a v24 Fidia iokoayo nafsi na shimo yaelekeza mbali zaidi ya maneno ya Elihu, kwenye fidia ambayo Baba yetu angeitoa siku moja katika Yesu, aliyeutoa uhai wake kuwa fidia ya wengi. 25ndipo nyama yake hupata upya kuliko ya mtoto; hurudia siku za ujana wake. 26Humwomba Mungu, naye anayemwabudu hukubaliwa naye; anayemwabudu hukiona uso wa Mungu kwa vigelegele vya furaha, naye Mungu humrudishia mtu huyo haki yake. 27Huimba mbele ya wengine na kusema, 'Nilitenda dhambi na kulipotosha lililo sawa, lakini sikulipwa kwalo. 28Aliikomboa nafsi yangu isishuke shimoni, nami nitauona mwanga.'
29"Tazama, Mungu hufanya mambo haya yote mara kwa mara na mtu, 30ili kuirudisha nafsi yake kutoka shimoni, apate kuangazwa kwa mwanga wa walio hai.
31"Zingatia, Ayubu; nisikilize. Nyamaza, nami nitasema. 32Kama una lo lote la kusema, nijibu; sema, kwa maana ningependa kukuona umehesabiwa haki. 33La sivyo, basi nisikilize; nyamaza, nami nitakufundisha hekima."