Walinzi Wawekwa kwenye Malango ya Yerusalemu
7 1Baada ya ukuta kujengwa upya na nikiisha kusimamisha milango, walinzi wa malango, waimbaji, na Walawi wakawekwa. 2Nikamweka ndugu yangu Hanani awe msimamizi wa Yerusalemu, pamoja na Hanania jemadari wa ngome, kwa kuwa alikuwa mtu mwaminifu na alimcha Baba yetu kuliko watu wengi. 3Nikawaambia, "Msiyafungue malango ya Yerusalemu mpaka jua liwe kali; na wakati walinzi wangali kwenye zamu, na wayafunge milango na kuyapiga makomeo. Wekeni walinzi kutoka miongoni mwa wakazi wa Yerusalemu, kila mmoja mahali pake, na kila mmoja mkabala wa nyumba yake mwenyewe."
4Mji ulikuwa mkubwa na wa nafasi, lakini watu waliokuwamo ndani yake walikuwa wachache, na hapakuwa na nyumba zilizojengwa upya.
Watu wa Baba Wahesabiwa Warudipo Nyumbani
5Ndipo Baba yangu akaweka moyoni mwangu kuwakusanya wakuu, na maafisa, na watu, ili waandikishwe kwa nasaba. Nikapata kitabu cha nasaba cha wale waliorudi kwanza, nikakuta kimeandikwa ndani yake:
6Hawa ndio watu wa jimbo waliorudi kutoka utumwani, ambao Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuwa amewachukua mateka, wakarudi Yerusalemu na Yuda, kila mmoja mjini kwake, 7waliokuja pamoja na Zerubabeli, Yeshua, Nehemia, Azaria, Raamia, Nahamani, Mordekai, Bilshani, Mispereti, Bigwai, Nehumu, na Baana—hesabu ya wanaume wa watu wa Israeli:
8Wazao wa Paroshi, 2,172;
9wazao wa Shefatia, 372;
10wazao wa Ara, 652;
11wazao wa Pahath-moabu (kwa ukoo wa Yeshua na Yoabu), 2,818;
12wazao wa Elamu, 1,254;
13wazao wa Zatu, 845;
14wazao wa Zakai, 760;
15wazao wa Binui, 648;
16wazao wa Bebai, 628;
17wazao wa Azgadi, 2,322;
18wazao wa Adonikamu, 667;
19wazao wa Bigwai, 2,067;
20wazao wa Adini, 655;
21wazao wa Ateri (kwa ukoo wa Hezekia), 98;
22wazao wa Hashumu, 328;
23wazao wa Besai, 324;
24wazao wa Harifu, 112;
25wazao wa Gibeoni, 95.
26Wanaume wa Bethlehemu na Netofa, 188;
27wanaume wa Anathothi, 128;
28wanaume wa Beth-azmavethi, 42;
29wanaume wa Kiriath-yearimu, Kefira, na Beerothi, 743;
30wanaume wa Rama na Geba, 621;
31wanaume wa Mikmasi, 122;
32wanaume wa Betheli na Ai, 123;
33wanaume wa Nebo ile nyingine, 52.
34Wazao wa Elamu ile nyingine, 1,254;
35wazao wa Harimu, 320;
36wazao wa Yeriko, 345;
37wazao wa Lodi, Hadidi, na Ono, 721;
38wazao wa Senaa, 3,930.
39Makuhani: wazao wa Yedaya (kwa nyumba ya Yeshua), 973.
40Wazao wa Imeri, 1,052;
41wazao wa Pashuri, 1,247;
42wazao wa Harimu, 1,017.
43Walawi: wazao wa Yeshua (kwa Kadmieli na ukoo wa Hodeva), 74.
44Waimbaji: wazao wa Asafu, 148.
45Walinzi wa malango: wazao wa Shalumu, Ateri, Talmoni, Akubu, Hatita, na Shobai, 138.
46Watumishi wa hekalu: wazao wa Siha, Hasufa, Tabaothi, 47Kerosi, Sia, Padoni, 48Lebana, Hagaba, Shalmai, 49Hanani, Gideli, Gahari, 50Reaya, Resini, Nekoda, 51Gazamu, Uza, Pasea, 52Besai, Meunimu, Nefushesimu, 53Bakbuki, Hakufa, Harhuri, 54Bazlithi, Mehida, Harsha, 55Barkosi, Sisera, Tema, 56Nesia, na Hatifa.
57Wazao wa watumishi wa Sulemani: wazao wa Sotai, Sofereti, Perida, 58Yaala, Darkoni, Gideli, 59Shefatia, Hatili, Pochereth-hazebaimu, na Amoni. 60Watumishi wote wa hekalu na wazao wa watumishi wa Sulemani walikuwa 392.
61Hawa ndio waliopanda kutoka Tel-mela, Tel-harsha, Kerubu, Adoni, na Imeri, lakini hawakuweza kuonyesha nyumba ya baba zao wala nasaba yao, kama walikuwa wa Israeli:
62Wazao wa Delaya, Tobia, na Nekoda, 642.
63Kutoka miongoni mwa makuhani: wazao wa Hobaya, Hakosi, na Barzilai—aliyeoa mmoja wa binti za Barzilai Mgileadi na akaitwa kwa jina la jamaa hiyo.
64Hawa wakatafuta kumbukumbu zao za nasaba, lakini hazikupatikana, kwa hiyo waliondolewa katika ukuhani kama walio najisi. 65Mtawala akawaambia wasile chakula kitakatifu zaidi hata atakapokuwepo kuhani wa kuuliza kwa Urimu na Thumimu. a a v65 Urimu na Thumimu vilikuwa vitu vitakatifu vilivyotunzwa na kuhani mkuu, vikitumika kutafuta uamuzi ulio wazi kutoka kwa Mungu juu ya mambo magumu.
66Kusanyiko lote pamoja lilikuwa na watu 42,360, 67mbali na watumishi wao wanaume na wanawake 7,337; nao walikuwa na waimbaji wanaume na wanawake 245. 68Walikuwa na farasi 736, nyumbu 245, 69ngamia 435, na punda 6,720.
70Baadhi ya vichwa vya jamaa walitoa kwa ajili ya kazi. Mtawala akatoa hazinani sarafu za dhahabu 1,000, mabakuli 50, na mavazi ya ukuhani 530. 71Baadhi ya vichwa vya jamaa wakatoa kwa hazina ya kazi sarafu za dhahabu 20,000 na kama ratili 2,750 za fedha. 72Watu wengine waliobaki wakatoa sarafu za dhahabu 20,000, kama ratili 2,500 za fedha, na mavazi ya ukuhani 67.
73Makuhani, Walawi, walinzi wa malango, waimbaji, baadhi ya watu, watumishi wa hekalu, na Israeli wote wakakaa katika miji yao. Ilipofika mwezi wa saba, watu wa Israeli walikuwa katika miji yao.