Wimbo wa kwenda juu. Wa Daudi.
Furaha ya mhiji anapofika nyumbani kwa Baba yetu, miguu yake ikiwa imesimama ndani ya malango. Mji ndipo makabila yanapokutana na haki inapotolewa, hivyo anauombea amani, na anasema anafanya hivyo kwa ajili ya ndugu zake, si yake mwenyewe.
122 1Nalifurahi pamoja na wale waliosema kwangu, "Na twende nyumbani kwa Baba yetu." 2Miguu yetu inasimama ndani ya malango yako, Ee Yerusalemu. 3Yerusalemu, uliojengwa kama mji ulioshikamana pamoja imara, 4ambako makabila hupanda, makabila ya Baba yetu, kama amri kwa Israeli, kulishukuru jina la Baba yetu. 5Kwa maana huko viti vya enzi vya hukumu viliwekwa, viti vya enzi vya nyumba ya Daudi.
6Iombeeni Yerusalemu amani: "Wapate raha wale wakupendao. 7Amani iwe ndani ya kuta zako, salama ndani ya ngome zako." 8Kwa ajili ya ndugu zangu na wenzangu, nitasema, "Amani iwe ndani yako." 9Kwa ajili ya nyumba ya Baba yetu nitakutafutia mema.